Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 4:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Baadaye, Yehova akamuuliza Kaini: “Yuko wapi Abeli ndugu yako?” naye akajibu: “Sijui. Kwani mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” 10 Basi Mungu akasema: “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia kwa sauti kutoka ardhini.+

  • Mwanzo 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Zaidi ya hayo, nitadai muwajibike kwa sababu ya damu ya uhai wenu.* Nitadai kila kiumbe aliye hai awajibike; nami nitamdai kila mwanadamu awajibike kwa sababu ya uhai wa ndugu yake.+

  • Kumbukumbu la Torati 32:43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,+

      Kwa maana atailipizia kisasi damu ya watumishi wake,+

      Atawalipiza kisasi maadui wake+

      Na kufunika dhambi ya* nchi ya watu wake.”

  • 2 Wafalme 9:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Yehu akachukua upinde wake na kumpiga mshale Yehoramu katikati ya mabega, na mshale huo ukatokea moyoni mwake, naye akaanguka ndani ya gari lake la vita.

  • 2 Wafalme 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 ‘“Kwa hakika kama nilivyoona damu ya Nabothi+ na damu ya wanawe jana,” asema Yehova, “nitakulipa+ wewe katika shamba hilihili,” asema Yehova.’ Basi sasa mwinue na umtupe katika shamba hili, kulingana na neno la Yehova.”+

  • 2 Wafalme 24:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Hakika watu wa Yuda walipatwa na mambo hayo kwa agizo la Yehova, ili kuwaondoa mbele za macho yake+ kwa sababu ya dhambi zote ambazo Manase alitenda,+ 4 na pia kwa sababu ya damu isiyo na hatia aliyomwaga,+ kwa maana alijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia na Yehova hakutaka kumsamehe.+

  • Luka 11:49-51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 49 Kwa sababu hiyo hekima ya Mungu ilisema: ‘Nitawatuma manabii na mitume kwao, lakini watawaua na kuwatesa baadhi yao, 50 ili damu ya manabii wote iliyomwagwa tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu idaiwe kutoka kwa kizazi hiki,+ 51 kuanzia damu ya Abeli+ mpaka damu ya Zekaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na ile nyumba.’*+ Ndiyo, ninawaambia, kizazi hiki kitadaiwa* damu hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki