-
Danieli 7:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 “Nikaendelea kutazama mpaka viti vya ufalme vikawekwa na Mzee wa Siku+ akaketi.+ Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji,+ na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha ufalme kilikuwa miali ya moto; magurudumu yake yalikuwa moto unaowaka.+ 10 Mto wa moto ulikuwa ukitiririka kutoka mbele zake.+ Elfu kwa maelfu waliendelea kumhudumia, na elfu kumi mara elfu kumi walisimama mbele zake.+ Mahakama+ ikaketi, na vitabu vikafunguliwa.
-