16 Ndipo Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji ili waimbe kwa shangwe na sauti kubwa, kwa ala za muziki: vinanda, vinubi,+ na matoazi.+
6 Hao wote walikuwa chini ya usimamizi wa baba yao wakiwa waimbaji katika nyumba ya Yehova, wakitumia matoazi, vinanda, na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.
Asafu, Yeduthuni, na Hemani walikuwa chini ya usimamizi wa mfalme.
25 Wakati huo, aliwaweka Walawi katika nyumba ya Yehova wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi,+ kulingana na amri ya Daudi+ na ya Gadi+ mwonaji wa mfalme na ya nabii Nathani,+ kwa maana amri hiyo ilitoka kwa Yehova kupitia manabii wake.