Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 9:18-20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia, kwa sababu wakuu wa Waisraeli walikuwa wamewaapia kwa jina la Yehova+ Mungu wa Israeli. Kwa hiyo Waisraeli wote wakaanza kuwanung’unikia wakuu hao. 19 Basi wakuu wote wakawaambia hivi: “Kwa kuwa tuliwaapia kwa jina la Yehova Mungu wa Israeli haturuhusiwi kuwadhuru. 20 Hili ndilo jambo tutakalofanya: Tutawaacha waishi, ili hasira ya Mungu isiwake dhidi yetu kwa sababu ya kiapo tulichowaapia.”+

  • Waamuzi 11:34, 35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Mwishowe Yeftha akafika nyumbani kwake Mispa,+ na tazama! binti yake akatoka ili kumpokea, huku akipiga tari na kucheza dansi! Naye alikuwa ndiye mtoto pekee. Yeftha hakuwa na mwana wala binti mwingine ila yeye. 35 Yeftha alipomwona, akararua mavazi yake na kusema, “Ole wangu, binti yangu! Umenivunja moyo,* kwa kuwa nimesababisha uende mbali. Nimetoa ahadi kwa Yehova, na siwezi kuivunja.”+

  • Zaburi 50:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+

      Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+

  • Mathayo 5:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 “Tena mlisikia kwamba zamani watu waliambiwa: ‘Usikose kutimiza kiapo chako,+ unapaswa kutimiza nadhiri zako kwa Yehova.’*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki