-
Yoshua 9:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia, kwa sababu wakuu wa Waisraeli walikuwa wamewaapia kwa jina la Yehova+ Mungu wa Israeli. Kwa hiyo Waisraeli wote wakaanza kuwanung’unikia wakuu hao. 19 Basi wakuu wote wakawaambia hivi: “Kwa kuwa tuliwaapia kwa jina la Yehova Mungu wa Israeli haturuhusiwi kuwadhuru. 20 Hili ndilo jambo tutakalofanya: Tutawaacha waishi, ili hasira ya Mungu isiwake dhidi yetu kwa sababu ya kiapo tulichowaapia.”+
-
-
Waamuzi 11:34, 35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 Mwishowe Yeftha akafika nyumbani kwake Mispa,+ na tazama! binti yake akatoka ili kumpokea, huku akipiga tari na kucheza dansi! Naye alikuwa ndiye mtoto pekee. Yeftha hakuwa na mwana wala binti mwingine ila yeye. 35 Yeftha alipomwona, akararua mavazi yake na kusema, “Ole wangu, binti yangu! Umenivunja moyo,* kwa kuwa nimesababisha uende mbali. Nimetoa ahadi kwa Yehova, na siwezi kuivunja.”+
-