-
Isaya 6:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Katika mwaka ambao Mfalme Uzia alikufa,+ nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme kilicho juu na kilichoinuliwa,+ na pindo za kanzu yake zilijaa hekaluni. 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita. Kila mmoja aliufunika uso wake kwa mabawa mawili na alifunika miguu yake kwa mawili, na kila mmoja wao aliruka huku na huku kwa mawili.
3 Na kila mmoja alimwambia mwenzake:
“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+
Dunia yote imejaa utukufu wake.”
-
-
Ezekieli 1:27, 28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Nami nikaona kitu kinachong’aa kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha,+ kilichokuwa kama moto unaong’aa kutoka kwenye kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kwenda juu; na kutoka kwenye kiuno chake kwenda chini, nikaona kitu kilichofanana na moto.+ Kulikuwa na mwangaza mkali kumzunguka pande zote 28 kama wa upinde wa mvua+ katika mawingu siku ya mvua. Hivyo ndivyo mwangaza uliozunguka pande zote ulivyoonekana. Ulikuwa kama mwonekano wa utukufu wa Yehova.+ Nilipouona, nikaanguka chini kifudifudi na kuanza kusikia sauti ya mtu akizungumza.
-
-
Ufunuo 4:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Baada ya hayo mara moja nikawa katika nguvu za roho, na tazama! kiti cha ufalme kilikuwa mahali pake mbinguni, na kulikuwa na mtu aliyeketi kwenye kile kiti.+ 3 Na Yule aliyeketi alionekana kama jiwe la yaspi+ na jiwe jekundu lenye thamani, na kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.+
-