-
Mwanzo 22:15-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Na malaika wa Yehova akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni, 16 akamwambia: “‘Naapa kwa nafsi yangu,’ asema Yehova,+ ‘kwamba kwa kuwa umetenda jambo hili nawe hujaninyima mwana wako, mwana wako wa pekee,+ 17 hakika nitakubariki, nami hakika nitaufanya uzao* wako uwe mwingi kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari,+ na uzao* wako utamiliki lango la* maadui wake.+ 18 Na kupitia uzao wako*+ mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umeisikiliza sauti yangu.’”+
-