Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 68:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Mungu huwapa makao walio peke yao;+

      Huwaachilia huru wafungwa na kuwafanikisha.+

      Lakini ni lazima watu wakaidi* waishi katika nchi iliyokauka.+

  • Zaburi 146:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Yeye anayetekeleza haki kwa ajili ya waliopunjwa,

      Yeye anayewapa chakula* wenye njaa.+

      Yehova anawaachilia huru wafungwa.*+

  • Isaya 49:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Yehova anasema hivi:

      “Wakati wa kibali* nilikujibu,+

      Na katika siku ya wokovu nilikusaidia;+

      Niliendelea kukulinda ili nikutoe uwe agano kwa ajili ya watu,+

      Ili kuitengeneza upya nchi,

      Ili kuwafanya wamiliki urithi wao ulio ukiwa,+

       9 Ili kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni nje!’+

      Na wale walio gizani,+ ‘Tokeni nje mwonekane!’

      Watalisha kando ya barabara,

      Malisho yao yatakuwa kando ya njia zilizokanyagwa.*

  • Isaya 61:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 61 Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu,+

      Kwa sababu Yehova alinitia mafuta niwatangazie wapole habari njema.+

      Alinituma kuyafunga majeraha ya waliovunjika moyo,

      Kuwatangazia mateka uhuru

      Na kutangaza kwamba macho ya wafungwa yatafunguliwa kabisa,+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki