5 Vivyo hivyo, pia Kristo hakujitukuza mwenyewe+ kwa kuwa kuhani mkuu, bali alitukuzwa na Yule aliyemwambia hivi: “Wewe ni mwanangu; leo nimekuwa baba yako.”+6 Kama vile pia anavyosema mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+
19 Tuna tumaini hilo+ kama nanga ya nafsi,* likiwa hakika na imara, nalo huingia ndani ya pazia,+20 ambamo mtangulizi ameingia kwa ajili yetu, Yesu,+ ambaye amekuwa kuhani mkuu milele kama Melkizedeki.+
11 Basi, ikiwa ukamilifu ungeweza kupatikana kupitia ukuhani wa Walawi+ (kwa maana ulikuwa sehemu ya Sheria ambayo watu walipewa), kungekuwa na umuhimu gani wa kuhani mwingine kusimama anayesemwa kuwa kwa mfano wa Melkizedeki+ na si kwa mfano wa Haruni?