Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa nini Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia ovu alipowatoa Misri. Alitaka kuwaua milimani na kuwaangamiza kabisa kutoka duniani’?+ Acha hasira yako inayowaka na ufikirie upya* uamuzi wako wa kuwaletea watu wako msiba huu.

  • Hesabu 14:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ukiwaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia sifa zako yatasema, 16 ‘Yehova alishindwa kuwapeleka watu hawa katika nchi ambayo aliapa kuwa angewapa ndiyo sababu aliwachinja nyikani.’+

  • Kumbukumbu la Torati 32:26, 27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Ningesema: “Nitawatawanya;

      Nitafanya ukumbusho wao usahauliwe kabisa miongoni mwa wanadamu,”

      27 Isingekuwa kwa sababu ya kuogopa jinsi maadui wangu watakavyotenda,+

      Kwa sababu huenda wapinzani wakalielewa vibaya jambo hilo.+

      Huenda wakasema: “Nguvu zetu zimeshinda;+

      Si Yehova aliyefanya mambo haya yote.”

  • Zaburi 79:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+

      Na ijulikane miongoni mwa mataifa mbele ya macho yetu

      Kwamba damu iliyomwagwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki