-
Kumbukumbu la Torati 17:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Atakapoketi kwenye kiti cha ufalme wake, ni lazima ajiandikie kwenye kitabu* nakala ya Sheria hii, kwa kutumia nakala inayowekwa na makuhani Walawi.+
19 “Anapaswa kubaki nacho, naye lazima akisome sikuzote za maisha yake,+ ili ajifunze kumwogopa Yehova Mungu wake na kushika maneno yote ya Sheria hii na masharti haya kwa kuyatekeleza.+ 20 Hivyo moyo wake hautajikweza juu ya ndugu zake, naye hataacha amri hiyo na kwenda kulia au kushoto, ili aendelee kutawala kwa muda mrefu katika ufalme wake, yeye na wanawe katika Israeli.
-