-
Waamuzi 13:22, 23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Kisha Manoa akamwambia hivi mke wake: “Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu.”+ 23 Lakini mke wake akamwambia, “Kama Yehova angetaka kutuua, hangekubali dhabihu ya kuteketezwa+ na toleo la nafaka kutoka mikononi mwetu, naye hangetuonyesha mambo haya yote, wala hangetuambia mambo haya yote.”
-
-
1 Samweli 25:30, 31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Na baada ya Yehova kukufanyia wewe bwana wangu mambo yote mema aliyoahidi na kukuweka kuwa kiongozi wa Israeli,+ 31 hutahuzunika wala kujuta moyoni mwako kwa sababu ya kumwaga damu bila sababu na kulipiza kisasi*+ kwa mkono wako bwana wangu. Yehova atakapokutendea mema bwana wangu, nikumbuke mimi kijakazi wako.”
-
-
Esta 5:8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Ikiwa nimepata kibali chako Ee mfalme, nawe mfalme ukipenda kutimiza ombi langu na kunipa ninachotaka, naomba mfalme uje pamoja na Hamani kwenye karamu ambayo nitawaandalia kesho; na kesho nitafanya kama unavyosema mfalme.”
-
-
Tito 2:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Vilevile wanawake wenye umri mkubwa wanapaswa kuwa wenye tabia ya kumhofu Mungu, wasiwe wachongezi, wala wasiwe watumwa wa divai nyingi, wawe walimu wa yaliyo mema;
-