-
1 Wafalme 21:20, 21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Ahabu akamwambia Eliya: “Yaani umenipata, ewe adui yangu?”+ Akajibu: “Nimekupata. ‘Kwa sababu umeazimia* kutenda maovu machoni pa Yehova,+ 21 sasa ninakuletea msiba, nami nitafagia kabisa baada yako na kumwangamiza kila mwanamume* wa Ahabu,+ kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli.+
-
-
1 Wafalme 22:8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Bado kuna mtu mmoja ambaye tunaweza kumwomba ushauri kutoka kwa Yehova;+ lakini ninamchukia,+ kwa maana hatabiri kamwe mambo mema kunihusu, ila mabaya tu.+ Anaitwa Mikaya mwana wa Imla.” Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme, usiseme jambo kama hilo.”
-
-
2 Mambo ya Nyakati 25:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Kwa hiyo Yehova akamkasirikia sana Amazia, akamtuma nabii ambaye alimwambia: “Kwa nini unaifuata miungu ya mataifa ambayo haikuwaokoa watu wake kutoka mikononi mwako?”+ 16 Nabii huyo alipokuwa akizungumza naye, mfalme akamwambia: “Je, tulikuweka uwe mshauri wa mfalme?+ Nyamaza!+ Kwa nini unataka kuuawa?” Ndipo nabii huyo akanyamaza, lakini akasema: “Najua kwamba Mungu ameamua kukuangamiza, kwa sababu umetenda hivyo na hujasikiliza ushauri wangu.”+
-