Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 33:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Baadaye Esau akasema: “Tuondoke, tufunge safari, acha nikutangulie.” 13 Lakini Yakobo akamwambia: “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni dhaifu+ nami nina kondoo na ng’ombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa haraka-haraka kwa siku moja, wanyama wote watakufa. 14 Tafadhali, bwana wangu, nitangulie mimi mtumishi wako, lakini nitaendelea na safari polepole kulingana na mwendo wa mifugo na watoto mpaka nitakapofika kwako bwana wangu huko Seiri.”+

  • Kutoka 23:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Kwa siku sita utafanya kazi zako; lakini siku ya saba hutafanya kazi, ili ng’ombe dume wako na punda wako wapumzike na mwana wa kijakazi wako na mkaaji mgeni waweze kujiburudisha.+

  • Kumbukumbu la Torati 22:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 “Ukimwona punda wa ndugu yako au ng’ombe dume wake akianguka barabarani hupaswi kumpuuza kimakusudi. Unapaswa kumsaidia kumwinua mnyama huyo.+

  • Kumbukumbu la Torati 22:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Usilime kwa ng’ombe dume na punda pamoja.+

  • Kumbukumbu la Torati 25:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe dume anapopura nafaka.+

  • Yona 4:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Je, mimi pia sipaswi kulihurumia jiji kubwa la Ninawi,+ ambalo lina watu zaidi ya 120,000 ambao hata hawajui kutofautisha jema na baya,* na kuwahurumia pia wanyama wao wengi?”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki