-
1 Samweli 2:22-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Sasa Eli alikuwa amezeeka sana, lakini alikuwa amesikia mambo yote ambayo wanawe walikuwa wakiwatendea+ Waisraeli wote na jinsi walivyokuwa wakilala na wanawake waliotumikia kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 23 Alikuwa akiwaambia hivi: “Kwa nini mnaendelea kufanya mambo ya aina hii? Kwa maana mambo ninayosikia kuwahusu kutoka kwa watu wote ni mabaya. 24 Msifanye hivyo wanangu, kwa sababu habari ninazosikia zikienea miongoni mwa watu wa Yehova si nzuri. 25 Mwanadamu akimtendea dhambi mwanadamu mwenzake, mtu fulani anaweza kumsihi Yehova kwa niaba yake;* lakini mwanadamu akimtendea dhambi Yehova,+ ni nani anayeweza kusali kwa ajili yake?” Lakini walikataa kumsikiliza baba yao, kwa sababu Yehova alikuwa ameazimia kuwaua.+
-
-
1 Samweli 8:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Samweli alipokuwa amezeeka, aliwaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli. 2 Mwana wake wa kwanza aliitwa Yoeli, na wa pili aliitwa Abiya;+ walikuwa waamuzi huko Beer-sheba. 3 Lakini wanawe hawakufuata njia zake; walikuwa na mwelekeo wa kujitafutia faida isiyo ya haki,+ walipokea rushwa,+ na kupotosha haki.+
-