-
Mhubiri 3:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 kwa maana kuna mwisho wa* wanadamu na mwisho wa wanyama; wote wana mwisho uleule.+ Anavyokufa huyu, ndivyo anavyokufa huyu; na wote wana roho ileile.+ Kwa hiyo mwanadamu si bora kuliko wanyama, kwa maana kila kitu ni ubatili. 20 Wote wanaenda mahali palepale.+ Wote wanatoka mavumbini,+ na wote wanarudi mavumbini.+
-
-
Mhubiri 9:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Wote huwa na mwisho uleule,*+ waadilifu na waovu,+ watu wema na safi na wale wasio safi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa dhabihu. Mtu mwema ni sawa na mtenda dhambi; mtu anayeapa ni sawa na yule anayejihadhari kuhusu kuapa. 3 Jambo hili linalohuzunisha hutukia chini ya jua: Kwa kuwa wote wana mwisho uleule,*+ moyo wa wanadamu umejaa pia uovu; na kuna wazimu moyoni mwao muda wote wa maisha yao, kisha wanakufa!*
-
-
Mhubiri 9:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Nimeona jambo lingine chini ya jua, ya kwamba sikuzote si wenye mbio wanaoshinda mbio, wala wenye nguvu hawashindi vita,+ wala wenye hekima hawapati chakula sikuzote, wala werevu hawawi na utajiri sikuzote,+ wala wenye ujuzi hawafanikiwi sikuzote,+ kwa sababu wakati na matukio yasiyotarajiwa* huwapata wote.
-