-
Mhubiri 2:4-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Nilianza kufanya mambo makubwa.+ Nikajijengea nyumba;+ Nikajipandia mashamba ya mizabibu.+ 5 Nikajitengenezea mashamba na bustani, na humo nikapanda miti ya matunda ya kila aina. 6 Nikajichimbia mabwawa ya maji, ili kumwagilia maji msitu wenye miti iliyokuwa ikisitawi. 7 Nikapata watumishi wa kiume na wa kike,+ na watumishi wengine walizaliwa nyumbani mwangu.* Pia, nilipata mifugo mingi—ng’ombe na kondoo na mbuzi+—kuliko mtu yeyote aliyenitangulia Yerusalemu. 8 Nikajikusanyia fedha na dhahabu,+ hazina za* wafalme na za mikoa.+ Nikajikusanyia waimbaji wa kiume na wa kike, na pia chanzo cha raha tele kwa wanaume—mwanamke, naam, wanawake wengi.
-