4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
5 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona;
6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia;
Zina pua, lakini haziwezi kunusa;
7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa;
Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoi sauti yoyote kwa koo zake.+
8 Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+
Na pia wote wanaozitumaini.+