Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 135:15-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,

      Kazi ya mikono ya mwanadamu.+

      16 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+

      Zina macho, lakini haziwezi kuona;

      17 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia.

      Hazina pumzi vinywani mwake.+

      18 Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+

      Na pia wote wanaozitumaini.+

  • Isaya 40:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Fundi hutengeneza sanamu,*

      Mfua chuma huifunika kwa dhahabu,+

      Naye huitengenezea mikufu ya fedha.

  • Isaya 46:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kuna wale wanaomwaga dhahabu kwa wingi kutoka kwenye mikoba yao;

      Wanapima fedha katika mizani.

      Wanamwajiri mfua chuma, naye huitengeneza kuwa mungu.+

      Kisha wanasujudu, naam, wanaiabudu.*+

  • Yeremia 10:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kwa maana desturi za mataifa ni udanganyifu.*

      Ni mti tu wa msituni uliokatwa,

      Uliochongwa kwa mikono ya fundi kwa kifaa chake.*+

       4 Wanaupamba kwa fedha na dhahabu+

      Wanaupigilia misumari kwa nyundo ili usianguke.+

  • Yeremia 10:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Wote hawatumii akili nao ni wajinga.+

      Mafundisho kutoka kwa mti ni udanganyifu* mtupu.+

       9 Mabamba ya fedha huletwa kutoka Tarshishi+ na dhahabu kutoka Ufazi,

      Kazi ya fundi, ya mikono ya mhunzi.

      Mavazi yao ni nyuzi za bluu na sufu ya zambarau.

      Vyote hutengenezwa na wafanyakazi stadi.

  • Matendo 19:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Sasa mnaona na kusikia kwamba si katika Efeso tu,+ bali pia katika karibu mkoa wote wa Asia, Paulo huyu ameushawishi umati mkubwa na kuwafanya wawe na maoni tofauti, akisema kwamba miungu iliyotengenezwa kwa mikono, kwa kweli si miungu.+

  • 1 Wakorintho 10:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Basi, niseme nini? Je, kile kilichotolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au je, sanamu ni kitu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki