Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezra 1:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi+ wa Uajemi, ili neno la Yehova lililosemwa na Yeremia+ litimie, Yehova aliichochea roho ya Mfalme Koreshi wa Uajemi atoe tangazo katika ufalme wake wote, ambalo pia aliliandika,+ akisema:

      2 “Mfalme Koreshi wa Uajemi anasema hivi: ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye ameniagiza nimjengee nyumba Yerusalemu, nchini Yuda.+

  • Isaya 41:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Nimemwinua mtu kutoka kaskazini, naye atakuja,+

      Kutoka upande wa mapambazuko ya jua,*+ atakayeliitia jina langu.

      Atawakanyaga-kanyaga watawala* kana kwamba wao ni udongo,+

      Kama mfinyanzi anayeukanyaga-kanyaga udongo wenye maji.

  • Isaya 45:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 45 Hivi ndivyo Yehova anavyomwambia mtiwa-mafuta wake, Koreshi,+

      Ambaye nimeushika mkono wake wa kulia+

      Ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+

      Kuwanyang’anya silaha* wafalme,

      Kufungua mbele yake milango yenye pande mbili,

      Hivi kwamba malango hayatafungwa:

  • Isaya 46:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ninamwita kutoka mashariki* ndege anayewinda,+

      Kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza uamuzi* wangu.+

      Nimesema, nami nitalitimiza.

      Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+

  • Danieli 10:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi, Danieli ambaye pia aliitwa Belteshaza+ alipewa ufunuo; na ujumbe wake ulikuwa wa kweli, nao ulihusu pambano kubwa. Naye alielewa ujumbe huo na kupewa uelewaji kuhusu mambo aliyokuwa ameona.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki