19 Tazama! Wakati huo nitawachukulia hatua wote wanaokukandamiza;+
Nami nitamwokoa yule anayechechemea,+
Nitawakusanya pamoja waliotawanyika.+
Nitawafanya kuwa kitu cha sifa na umaarufu
Katika kila nchi ambamo waliaibishwa.
20 Wakati huo nitawaleta ndani,
Wakati nitakapowakusanya pamoja.
Kwa maana nitawafanya kuwa kitu cha umaarufu na sifa+ miongoni mwa mataifa yote duniani,
Nitakapowakusanya mateka wenu mbele ya macho yenu,” asema Yehova.+