Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 61:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa maana kama dunia inavyochipusha mimea

      Na kama bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa humo,

      Ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova

      Atakavyofanya uadilifu+ na sifa zichipuke+ mbele ya mataifa yote.

  • Yeremia 33:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Naye atakuwa kwangu jina la furaha, sifa, na uzuri mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia kuhusu wema wote nitakaowapa.+ Nao wataogopa na kutetemeka+ kwa sababu ya wema na amani ninayompa.’”+

  • Sefania 3:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Tazama! Wakati huo nitawachukulia hatua wote wanaokukandamiza;+

      Nami nitamwokoa yule anayechechemea,+

      Nitawakusanya pamoja waliotawanyika.+

      Nitawafanya kuwa kitu cha sifa na umaarufu*

      Katika kila nchi ambamo waliaibishwa.

      20 Wakati huo nitawaleta ndani,

      Wakati nitakapowakusanya pamoja.

      Kwa maana nitawafanya kuwa kitu cha umaarufu* na sifa+ miongoni mwa mataifa yote duniani,

      Nitakapowakusanya mateka wenu mbele ya macho yenu,” asema Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki