Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 30:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+ 2 nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+

  • Isaya 11:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Na kutakuwa na barabara kuu+ kutoka Ashuru kwa ajili ya watu wake waliobaki,+

      Kama ilivyokuwa kwa ajili ya Israeli siku aliyotoka nchini Misri.

  • Isaya 43:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’+

      Na kusini, ‘Usiwazuie.

      Walete wanangu kutoka mbali, na mabinti wangu kutoka kwenye miisho ya dunia,+

  • Isaya 60:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Inua macho yako utazame pande zote kukuzunguka!

      Wote wamekusanywa; wanakuja kwako.

      Wana wako wanaendelea kuja kutoka mbali sana,+

      Na mabinti wako wakiwa wametegemezwa viunoni.+

  • Isaya 60:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Kwa maana visiwa vitanitumaini;+

      Meli za Tarshishi zinaongoza,*

      Kuwaleta wana wako kutoka mbali sana,+

      Pamoja na fedha yao na dhahabu yao,

      Kwa sifa ya jina la Yehova Mungu wako na ya Mtakatifu wa Israeli,

      Kwa maana atakutukuza.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki