Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 19:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Siku hiyo kutakuwa na barabara kuu+ kutoka Misri kwenda Ashuru. Kisha Ashuru itakuja Misri, na Misri itaenda Ashuru; na Misri itamtumikia Mungu pamoja na Ashuru.

  • Isaya 27:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Siku hiyo pembe kubwa itapigwa,+ na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru+ na wale waliotawanywa katika nchi ya Misri+ watakuja na kumwinamia Yehova kwenye mlima mtakatifu huko Yerusalemu.+

  • Isaya 35:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Na huko kutakuwa na barabara kuu,+

      Naam, njia inayoitwa Njia ya Utakatifu.

      Mtu asiye safi hatasafiri kwenye njia hiyo.+

      Imetengwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo;

      Hakuna mtu yeyote mpumbavu atakayepotea na kuingia katika njia hiyo.

  • Isaya 40:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kuna mtu anayepaza sauti nyikani:

      “Fungueni* njia ya Yehova!+

      Tengenezeni barabara kuu iliyonyooka+ inayopitia jangwani kwa ajili ya Mungu wetu.+

  • Isaya 57:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Itasemwa, ‘Tengenezeni, tengenezeni barabara! Tayarisheni njia!+

      Ondoeni kizuizi chochote katika njia ya watu wangu.’”

  • Yeremia 31:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “Jiwekee alama za barabara,

      Na uweke vibao vya ishara.+

      Kazia fikira barabara kuu, njia ambayo unapaswa kupitia.+

      Rudi, ewe bikira wa Israeli, rudi kwenye majiji haya yako.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki