-
Marko 1:2-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya: “(Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele yako,* ili akutayarishie njia.)+ 3 Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.’”+ 4 Yohana Mbatizaji alikuwa nyikani, akiwahubiria watu wabatizwe ili kuonyesha kwamba wametubu na hivyo wasamehewe dhambi zao.+
-
-
Luka 3:3-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi akaenda katika maeneo yote yaliyokuwa karibu na Yordani, akiwahubiria watu wabatizwe ili kuonyesha kwamba wametubu na hivyo wasamehewe dhambi zao,+ 4 kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya nabii Isaya: “Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.+ 5 Lazima kila bonde lijazwe, na kila mlima na kilima visawazishwe; lazima barabara zilizopinda zinyooshwe, na barabara zenye miparuzo zilainishwe; 6 na wote wenye mwili* wataona wokovu wa Mungu.’”*+
-