Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+

  • Hosea 7:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kiburi cha Waisraeli kimetoa ushahidi dhidi yao,+

      Lakini hawajamrudia Yehova Mungu wao,+

      Wala hawajamtafuta licha ya hayo yote.

  • Amosi 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 ‘Lakini mimi niliyafanya meno yenu yawe safi bila chakula* katika majiji yenu yote

      Nikasababisha mkose mikate katika nyumba zenu zote;+

      Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.

  • Amosi 5:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Mtafuteni Yehova, mwendelee kuishi,+

      Ili asilipuke kama moto kwenye nyumba ya Yosefu,

      Na kuteketeza kabisa Betheli, hivi kwamba hakuna mtu atakayeweza kuuzima moto huo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki