Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 30:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+ 2 nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+

  • Isaya 66:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ wawe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari ya vita, ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa, juu ya nyumbu, juu ya ngamia wenye kasi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu, Yerusalemu,” asema Yehova, “kama watu wa Israeli wanavyoleta zawadi zao ndani ya nyumba ya Yehova zikiwa katika chombo safi.”

  • Yeremia 24:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Jicho langu litaendelea kuwatazama kwa faida yao, nami nitawarudisha katika nchi hii.+ Nitawajenga, nami sitawabomoa; nitawapanda, nami sitawang’oa.+

  • Ezekieli 36:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Nitawatoa kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi zote na kuwaleta katika nchi yenu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki