Zaburi 33:11 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Lakini maamuzi* ya Yehova yatasimama milele;+Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi baada ya kizazi. Methali 19:21 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 21 Moyo wa mwanadamu una mipango mingi,Lakini shauri* la Yehova ndilo litakalodumu.+ Methali 21:30 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+ Isaya 46:11 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Ninamwita kutoka mashariki* ndege anayewinda,+Kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza uamuzi* wangu.+ Nimesema, nami nitalitimiza. Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+
11 Ninamwita kutoka mashariki* ndege anayewinda,+Kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza uamuzi* wangu.+ Nimesema, nami nitalitimiza. Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+