-
Isaya 20:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha Yehova akasema: “Kama mtumishi wangu Isaya alivyotembea akiwa uchi na bila viatu kwa miaka mitatu ili kuwa ishara+ na dalili dhidi ya Misri+ na dhidi ya Ethiopia,+ 4 hivyo ndivyo mfalme wa Ashuru atakavyowaongoza mateka wa Misri+ na wahamishwa wa Ethiopia, wavulana na wanaume wazee, wakiwa uchi na bila viatu na matako yakiwa wazi, uchi wa* Misri.
-
-
Yeremia 43:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Tazameni, ninamwita Nebukadneza* mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, naye atalitandaza hema lake la kifalme juu yake.+ 11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa hatari atakufa kwa ugonjwa hatari, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga atakufa kwa upanga.+
-