Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 19:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kisha Musa akapanda mlimani kwa Mungu wa kweli, naye Yehova akamwita kutoka mlimani,+ akamwambia: “Hivi ndivyo utakavyoiambia nyumba ya Yakobo na kuwaambia Waisraeli,

  • Kutoka 19:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Sasa ikiwa mtaitii kabisa sauti yangu na kushika agano langu, hakika mtakuwa mali yangu ya pekee* kati ya mataifa yote,+ kwa maana dunia yote ni mali yangu.+

  • Kutoka 24:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Halafu akachukua kitabu cha agano na kuwasomea watu kwa sauti.+ Nao wakasema: “Mambo yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya, nasi tutatii.”+

  • Yeremia 31:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ ‘agano langu ambalo walilivunja,+ ingawa nilikuwa bwana* wao wa kweli,’ asema Yehova.”

  • Yeremia 34:18-20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Na hivi ndivyo itakavyokuwa kwa watu waliolivunja agano langu kwa kutofuata maneno ya agano walilofanya mbele zangu walipomkata ndama vipande viwili na kupita kati ya vile vipande viwili,+ 19 yaani, wakuu wa Yuda, wakuu wa Yerusalemu, maofisa wa makao ya mfalme, makuhani, na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande viwili vya ndama: 20 Nitawatia mikononi mwa maadui wao na mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua,* na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na cha wanyama wa dunia.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki