Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 9:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa;+

      Atayahukumu mataifa kwa kutoa maamuzi ya uadilifu.+

  • Zaburi 58:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ameona kisasi;+

      Miguu yake italowa damu ya waovu.+

      11 Kisha watu watasema: “Kwa hakika kuna thawabu kwa ajili ya mwadilifu.+

      Kwa hakika kuna Mungu anayehukumu duniani.”+

  • Zaburi 85:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Uaminifu utachipuka duniani,

      Na uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+

  • Zaburi 85:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Uadilifu utatembea mbele zake+

      Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

  • Zaburi 96:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,*

      Anakuja kuihukumu dunia.

      Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+

      Na mataifa kwa uaminifu wake.+

  • Zaburi 97:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+

      Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chake cha ufalme.+

  • Isaya 61:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa maana kama dunia inavyochipusha mimea

      Na kama bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa humo,

      Ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova

      Atakavyofanya uadilifu+ na sifa zichipuke+ mbele ya mataifa yote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki