Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 1:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Wakuu wako ni wakaidi na wanashirikiana na wezi.+

      Kila mmoja wao anapenda rushwa na kutafuta zawadi kwa bidii.+

      Hawawatendei kwa haki mayatima,

      Na kesi ya mjane haiwafikii kamwe.+

  • Yeremia 5:26-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Kwa maana kati ya watu wangu kuna watu waovu.

      Wanaendelea kuchungulia, kama wawindaji wa ndege wanapochutama.

      Wanatega mtego hatari.

      Wanawanasa watu.

      27 Kama kizimba kilichojaa ndege,

      Ndivyo nyumba zao zilivyojaa udanganyifu.+

      Ndiyo sababu wamekuwa wenye nguvu na matajiri.

      28 Wamenenepa na kuwa laini;

      Wanafurika uovu.

      Hawawatetei mayatima katika kesi,+

      Wanatafuta mafanikio yao wenyewe;

      Nao wanawanyima haki maskini.’”+

  • Mika 2:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Ole wao wanaopanga njama yenye kudhuru,

      Wanaotunga maovu vitandani mwao!

      Kunapopambazuka wanayatekeleza,

      Kwa sababu wana uwezo wa kuyatekeleza.+

       2 Wanatamani mashamba na kuyanyakua;+

      Pia nyumba, na kuzichukua;

      Wanamlaghai mtu na kuchukua nyumba yake,+

      Wanachukua urithi wa mtu.

  • Mika 6:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Je, bado kuna hazina za uovu katika nyumba ya mwovu

      Na kipimo kilichopunguka cha efa* kinachochukiza?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki