26 Kwa maana kati ya watu wangu kuna watu waovu.
Wanaendelea kuchungulia, kama wawindaji wa ndege wanapochutama.
Wanatega mtego hatari.
Wanawanasa watu.
27 Kama kizimba kilichojaa ndege,
Ndivyo nyumba zao zilivyojaa udanganyifu.+
Ndiyo sababu wamekuwa wenye nguvu na matajiri.
28 Wamenenepa na kuwa laini;
Wanafurika uovu.
Hawawatetei mayatima katika kesi,+
Wanatafuta mafanikio yao wenyewe;
Nao wanawanyima haki maskini.’”+