Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 25:8-10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi huo, yaani, mwaka wa 19 wa utawala wa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babiloni, alikuja Yerusalemu.+ 9 Akateketeza kabisa nyumba ya Yehova,+ nyumba ya mfalme,*+ na nyumba zote Yerusalemu;+ aliteketeza pia nyumba ya kila mtu maarufu.+ 10 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi lilibomoa kuta zilizozunguka Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:24, 25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “Yehova anasema, ‘Nitaleta msiba mahali hapa na kwa wakaaji wake,+ laana zote zilizoandikwa katika kitabu+ walichosoma mbele ya mfalme wa Yuda. 25 Kwa sababu wameniacha+ na wanaifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu ili kunikasirisha+ kwa kazi zote za mikono yao, ghadhabu yangu itamwagika mahali hapa nayo haitazimwa.’”+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.

      17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+

  • Maombolezo 2:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Ameukunja* upinde wake kama adui; mkono wake wa kuume uko tayari kama adui;+

      Aliendelea kuwaua wote wanaotamanika machoni.+

      Naye aliimwaga ghadhabu yake kama moto+ katika hema la binti ya Sayuni.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki