-
Yeremia 42:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Na watu wote walioazimia kwenda Misri ili kukaa huko watakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari. Hakuna yeyote kati yao atakayeokoka au kuponyoka msiba nitakaowaletea.”’
18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu ikiwa mtaenda Misri, nanyi mtakuwa laana, kitu cha kutisha, matusi, na shutuma,+ nanyi hamtapaona tena kamwe mahali hapa.’
-