43 Sasa hivi ndivyo anavyosema Yehova,
Muumba wako, Ee Yakobo, Yule aliyekuumba, Ee Israeli:+
“Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+
Nimekuita kwa jina lako.
Wewe ni mali yangu.
2 Unapopita katika maji, nitakuwa pamoja nawe,+
Na unapopita katika mito, haitafurika na kukufunika.+
Unapotembea katika moto, hutateketea,
Wala mwali wa moto hautakuunguza.