-
Yeremia 18:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Wakati wowote nitakaposema kuhusu kung’oa na kubomoa na kuharibu taifa au ufalme,+ 8 na taifa hilo liache uovu wake niliotangaza dhidi yake, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu msiba niliokusudia kuuleta dhidi yake.+ 9 Lakini wakati wowote ninaposema kuhusu kujenga na kupanda taifa au ufalme, 10 na taifa hilo litende maovu machoni pangu na kukosa kuitii sauti yangu, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu mema niliyokusudia kulitendea.’
-
-
Yeremia 24:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kama hizi tini nzuri, ndivyo nitakavyowaona kwa njia nzuri wale watu wa Yuda waliohamishwa, ambao nimewatoa mahali hapa na kuwapeleka katika nchi ya Wakaldayo. 6 Jicho langu litaendelea kuwatazama kwa faida yao, nami nitawarudisha katika nchi hii.+ Nitawajenga, nami sitawabomoa; nitawapanda, nami sitawang’oa.+
-