Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 8:33, 34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 “Watu wako Waisraeli wakishindwa na maadui kwa sababu ya kuzidi kukutendea dhambi,+ nao warudi kwako na kulitukuza jina lako+ na kusali na kukusihi wapate kibali katika nyumba hii,+ 34 basi usikie kutoka mbinguni na kuwasamehe watu wako Waisraeli dhambi yao na kuwarudisha katika nchi uliyowapa mababu zao.+

  • Zaburi 106:45
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 45 Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,

      Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+

  • Yeremia 7:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Rekebisheni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaruhusu mwendelee kukaa mahali hapa.+

  • Yeremia 26:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Labda watasikiliza na kila mmoja ataiacha njia yake ovu, nami nitabadili nia yangu* kuhusu msiba ninaokusudia kuwaletea kwa sababu ya matendo yao maovu.+

  • Ezekieli 18:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “‘Sasa mtu mwovu akiziacha dhambi zote alizofanya na kushika amri zangu na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, kwa hakika ataendelea kuishi. Hatakufa.+

  • Yoeli 2:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu,+

      Nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu,

      Kwa maana ni mwenye huruma* na rehema, si mwepesi wa hasira,+ naye ana upendo mwingi mshikamanifu,+

      Naye atafikiria upya* msiba aliokusudia kuleta.

  • Yona 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu,+ nao wakatangaza watu wafunge na kuvaa magunia, kuanzia aliye mkubwa zaidi hadi aliye mdogo zaidi.

  • Yona 3:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Mungu wa kweli alipoona waliyofanya, jinsi walivyoacha njia zao ovu,+ akafikiria upya kuhusu* msiba aliosema kwamba angewaletea, naye hakuuleta.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki