-
Ezekieli 18:21-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 “‘Sasa mtu mwovu akiziacha dhambi zote alizofanya na kushika amri zangu na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, kwa hakika ataendelea kuishi. Hatakufa.+ 22 Hatahukumiwa kwa kosa lolote alilotenda.*+ Ataendelea kuishi kwa kutenda uadilifu.’+
23 “‘Je, ninafurahia hata kidogo kifo cha mtu mwovu?’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Je, sipendelei kwamba aziache njia zake naye aendelee kuishi?’+
-
-
Yona 4:2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Basi akasali hivi kwa Yehova: “Ee Yehova, je, sikujua utafanya jambo hili nilipokuwa katika nchi yangu? Ndiyo sababu tangu awali nilijaribu kukimbilia Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema, hukasiriki upesi, una upendo mwingi mshikamanifu,+ na unahuzunishwa na msiba.
-