Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 18:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wakati wowote nitakaposema kuhusu kung’oa na kubomoa na kuharibu taifa au ufalme,+ 8 na taifa hilo liache uovu wake niliotangaza dhidi yake, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu msiba niliokusudia kuuleta dhidi yake.+

  • Ezekieli 18:21-23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “‘Sasa mtu mwovu akiziacha dhambi zote alizofanya na kushika amri zangu na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, kwa hakika ataendelea kuishi. Hatakufa.+ 22 Hatahukumiwa kwa kosa lolote alilotenda.*+ Ataendelea kuishi kwa kutenda uadilifu.’+

      23 “‘Je, ninafurahia hata kidogo kifo cha mtu mwovu?’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Je, sipendelei kwamba aziache njia zake naye aendelee kuishi?’+

  • Yona 4:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Basi akasali hivi kwa Yehova: “Ee Yehova, je, sikujua utafanya jambo hili nilipokuwa katika nchi yangu? Ndiyo sababu tangu awali nilijaribu kukimbilia Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema, hukasiriki upesi, una upendo mwingi mshikamanifu,+ na unahuzunishwa na msiba.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki