Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 136:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Aliziumba mbingu kwa ustadi,*+

      Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

  • Methali 3:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Yehova aliuweka msingi wa dunia kwa hekima.+

      Aliziimarisha kabisa mbingu kwa utambuzi.+

  • Isaya 40:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kuna Yule anayekaa juu ya duara ya* dunia,+

      Na wakaaji wake ni kama panzi.

      Anazitandaza mbingu kama wavu laini,

      Naye huzitandaza kama hema la kuishi.+

  • Yeremia 10:12-16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yeye ndiye Muumba wa dunia kwa nguvu zake,

      Yule aliyeiimarisha ardhi inayozaa kwa hekima yake+

      Na aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.+

      13 Anapofanya sauti yake isikike,

      Maji yaliyo mbinguni husukasuka,+

      Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.+

      Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua,

      Naye huutoa upepo katika maghala yake.+

      14 Kila mtu anatenda bila kutumia akili na bila ujuzi.

      Kila fundi wa chuma ataaibishwa kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+

      Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uwongo,

      Nazo hazina roho* ndani yake.+

      15 Sanamu hizo ni udanganyifu,* kazi ya mzaha.+

      Siku yao ya hukumu itakapofika, zitaangamia.

      16 Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,

      Kwa maana Yeye ndiye aliyeumba kila kitu,

      Na Israeli ndiyo fimbo ya urithi wake.+

      Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki