-
Isaya 40:22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Anazitandaza mbingu kama wavu laini,
Naye huzitandaza kama hema la kuishi.+
-
-
Yeremia 10:12-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Yeye ndiye Muumba wa dunia kwa nguvu zake,
Yule aliyeiimarisha ardhi inayozaa kwa hekima yake+
Na aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.+
13 Anapofanya sauti yake isikike,
Maji yaliyo mbinguni husukasuka,+
Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.+
14 Kila mtu anatenda bila kutumia akili na bila ujuzi.
Kila fundi wa chuma ataaibishwa kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+
Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uwongo,
15 Sanamu hizo ni udanganyifu,* kazi ya mzaha.+
Siku yao ya hukumu itakapofika, zitaangamia.
16 Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,
Kwa maana Yeye ndiye aliyeumba kila kitu,
Na Israeli ndiyo fimbo ya urithi wake.+
Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+
-