-
Kumbukumbu la Torati 12:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 “Yehova Mungu wenu atakapoyaangamiza mataifa ambayo mtamiliki nchi yao,+ na mtakapokuwa mkiishi katika nchi yao, 30 jihadharini msinaswe baada ya mataifa hayo kuangamizwa kutoka mbele yenu. Msiulize hivi kuhusu miungu yao: ‘Mataifa haya yaliabuduje miungu yake? Mimi pia nitafanya vivyo hivyo.’+ 31 Msimfanyie hivyo Yehova Mungu wenu, kwa sababu mataifa hayo yanaifanyia miungu yao kila jambo linalochukiza ambalo Yehova anachukia, hata kuwateketeza motoni wana na mabinti wao kwa ajili ya miungu yao.+
-
-
Ezekieli 20:31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Na je, bado mnajichafua mpaka leo hii kwa kuzitolea dhabihu sanamu zenu zote zinazochukiza, mkiwateketeza* motoni wana wenu?+ Je, wakati huohuo ninapaswa kujibu maombi yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+
“‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Sitajibu maombi yenu.+
-