Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 12:29-31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 “Yehova Mungu wenu atakapoyaangamiza mataifa ambayo mtamiliki nchi yao,+ na mtakapokuwa mkiishi katika nchi yao, 30 jihadharini msinaswe baada ya mataifa hayo kuangamizwa kutoka mbele yenu. Msiulize hivi kuhusu miungu yao: ‘Mataifa haya yaliabuduje miungu yake? Mimi pia nitafanya vivyo hivyo.’+ 31 Msimfanyie hivyo Yehova Mungu wenu, kwa sababu mataifa hayo yanaifanyia miungu yao kila jambo linalochukiza ambalo Yehova anachukia, hata kuwateketeza motoni wana na mabinti wao kwa ajili ya miungu yao.+

  • 2 Wafalme 17:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Pia waliwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao,+ wakafanya uaguzi,*+ wakatafuta ishara za ubashiri, na wakaendelea kujitoa* wenyewe kutenda maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.

  • 2 Mambo ya Nyakati 28:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Ahazi+ alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Hakutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova kama alivyotenda Daudi babu yake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 28:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Isitoshe, alifukiza moshi wa dhabihu katika Bonde la Mwana wa Hinomu* na kuwateketeza wanawe motoni,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 55 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na pia aliwateketeza* motoni wanawe mwenyewe+ katika Bonde la Mwana wa Hinomu;+ alifanya uchawi,+ alifanya uaguzi,* alifanya ulozi, na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.

  • Ezekieli 20:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Na je, bado mnajichafua mpaka leo hii kwa kuzitolea dhabihu sanamu zenu zote zinazochukiza, mkiwateketeza* motoni wana wenu?+ Je, wakati huohuo ninapaswa kujibu maombi yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+

      “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Sitajibu maombi yenu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki