Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 65:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wakaidi,+

      Wale wanaotembea katika njia isiyo nzuri,+

      Wanaofuata mawazo yao wenyewe;+

  • Yeremia 7:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao;+ badala yake walitembea katika mipango yao* wenyewe, wakifuata kwa ukaidi moyo wao mwovu,+ nao wakarudi nyuma, badala ya kwenda mbele,

  • Yeremia 7:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Lakini walikataa kunisikiliza, nao hawakutega sikio lao.+ Badala yake, walikuwa wakaidi,* nao walitenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zao!

  • Ezekieli 20:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “‘“Lakini wakaniasi nao hawakutaka kunisikiliza. Hawakuvitupa vitu vinavyochukiza vilivyokuwa mbele yao, nao walikataa kuziacha sanamu zinazochukiza za Misri.+ Basi nikaahidi kuwamwagia ghadhabu yangu na kuwaletea hasira yangu yote nchini Misri.

  • Zekaria 7:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ wakageuza migongo yao kwa ukaidi,+ na kuziba masikio yao ili wasisikie.+ 12 Waliifanya mioyo yao iwe kama almasi*+ nao walikataa kutii sheria* na maneno ambayo Yehova wa majeshi aliwapa kwa roho yake kupitia manabii wa kale.+ Kwa hiyo Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki