- 
	                        
            
            Yeremia 8:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
8 “Wakati huo,” asema Yehova, “mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakuu wake, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii, na mifupa ya wakaaji wa Yerusalemu itatolewa katika makaburi yao. 2 Itatandazwa juani na mbele ya mwezi na kwa jeshi lote la mbinguni ambalo wamelipenda na kulitumikia na kulifuata na kulitafuta na kuliinamia.+ Haitakusanywa, wala haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya ardhi.”+
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Sefania 1:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
4 “Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya watu wa Yuda
Na dhidi ya wakaaji wote wa Yerusalemu,
Nami nitafutilia mbali kutoka mahali hapa kila kitu kinachohusiana na* Baali,+
Jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani wenyewe,+
5 Na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni wakiwa juu ya paa,+
Na wale wanaoinama chini na kuapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Yehova+
Na wakati uleule wakiapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
 
 -