-
Yeremia 27:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Pia nilimwambia Mfalme Sedekia+ wa Yuda maneno hayohayo, nikisema: “Wekeni shingo zenu chini ya nira ya mfalme wa Babiloni na mumtumikie yeye na watu wake, nanyi mtaendelea kuishi.+ 13 Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga,+ kwa njaa kali,+ na kwa ugonjwa hatari,+ kama Yehova alivyosema kuhusu taifa ambalo halitamtumikia mfalme wa Babiloni?
-