Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 28:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Na hawa pia wanapotea njia kwa sababu ya divai;

      Wanapepesuka kwa sababu ya vileo vyao.

      Kuhani na nabii wanapotea njia kwa sababu ya kileo;

      Divai inawavuruga,

      Nao wanapepesuka kwa sababu ya kileo chao;

      Maono yao yanawafanya wapotee njia,

      Nao wanajikwaa wanapohukumu.+

  • Yeremia 5:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Manabii wanatabiri uwongo,+

      Nao makuhani wanakandamiza kwa mamlaka yao wenyewe.

      Na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo.+

      Lakini mtafanya nini mwisho ukifika?”

  • Yeremia 6:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+

      Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+

  • Ezekieli 22:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Ndani yake manabii wake wamepanga njama,+ kama simba anayenguruma akirarua mawindo.+ Wanawanyafua watu. Wanachukua hazina na vitu vyenye thamani. Wamewafanya wengi kuwa wajane ndani yake.

  • Sefania 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Manabii wake ni wakaidi, wanaume wenye hila.+

      Makuhani wake wanachafua kilicho kitakatifu;+

      Wanaitendea sheria kikatili.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki