Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 2:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Makuhani hawakuuliza, ‘Yehova yuko wapi?’+

      Wale wanaoshughulika na Sheria hawakunijua,

      Wachungaji waliniasi,+

      Manabii walitabiri kupitia Baali,+

      Nao wakawafuata wale ambao hawangewafaidi hata kidogo.

  • Yeremia 8:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Basi nitawapa wanaume wengine wake zao,

      Na mashamba yao nitawapa wamiliki wengine;+

      Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+

      Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+

      11 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la binti ya watu wangu, wakisema,

      “Kuna amani! Kuna amani!”

      Wakati hakuna amani.+

      12 Je, wanaona aibu kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza waliyotenda?

      Hawaoni aibu hata kidogo!

      Hata hawajui jinsi ya kufedheheka!+

      Basi wataanguka kati ya wale walioanguka.

      Nitakapowaletea adhabu watajikwaa,”+ asema Yehova.

  • Yeremia 23:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Nabii pamoja na kuhani wamechafuliwa.*+

      Hata katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata uovu wao,”+ asema Yehova.

  • Mika 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Yehova anasema hivi kuhusu manabii wanaowapotosha watu wake,+

      Wanaotangaza ‘Amani!’+ huku wakitafuna* kwa meno yao+

      Lakini wanaotangaza* vita dhidi ya yule asiyeweka kitu vinywani mwao:

  • Mika 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Viongozi* wake huhukumu ili wapate rushwa,+

      Makuhani wake hufundisha ili wapate malipo,+

      Na manabii wake hufanya uaguzi* ili wapate pesa.*+

      Na bado wanamwegemea Yehova,* wakisema:

      “Je, Yehova hayuko pamoja nasi?+

      Hakuna msiba utakaotupata.”+

  • Sefania 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Manabii wake ni wakaidi, wanaume wenye hila.+

      Makuhani wake wanachafua kilicho kitakatifu;+

      Wanaitendea sheria kikatili.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki