-
Yeremia 8:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Basi nitawapa wanaume wengine wake zao,
Na mashamba yao nitawapa wamiliki wengine;+
Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+
Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+
11 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la binti ya watu wangu, wakisema,
“Kuna amani! Kuna amani!”
Wakati hakuna amani.+
12 Je, wanaona aibu kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza waliyotenda?
Hawaoni aibu hata kidogo!
Hata hawajui jinsi ya kufedheheka!+
Basi wataanguka kati ya wale walioanguka.
Nitakapowaletea adhabu watajikwaa,”+ asema Yehova.
-