16 Yehova wa majeshi anasema hivi:
“Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatabiria ninyi.+
Wanawadanganya.
Wanasema maono ya moyo wao wenyewe,+
Si kutoka katika kinywa cha Yehova.+
17 Wanawaambia tena na tena wale wasioniheshimu,
‘Yehova amesema hivi: “Mtakuwa na amani.”’+
Nao wanamwambia kila mtu anayefuata moyo wake mkaidi,
‘Hutapatwa na msiba wowote.’+