14 Kisha Yehova akaniambia: “Manabii wanatabiri uwongo katika jina langu.+ Sikuwatuma wala kuwaamuru wala kuzungumza nao.+ Wanawatabiria ninyi maono ya uwongo na uaguzi* usiofaa kitu na udanganyifu wa moyo wao wenyewe.+
28 Lakini manabii wake wamepiga lipu matendo yao kwa kutumia chokaa. Wanaona maono ya uwongo na kufanya uaguzi* wa uwongo,+ nao wanasema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema.