-
Ezekieli 13:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Mkono wangu uko dhidi ya manabii ambao maono yao ni ya uwongo na wanaotabiri uwongo.+ Nao hawatakuwa miongoni mwa watu ninaowaambia siri zangu; wala hawataandikwa katika orodha ya watu wa nyumba ya Israeli; wala hawatarudi katika nchi ya Israeli; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ 10 Hayo yote ni kwa sababu wamewapotosha watu wangu wakisema, “Kuna amani!” wakati hakuna amani.+ Ukuta dhaifu unapojengwa, wanaupiga lipu kwa chokaa.’*+
-