Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 5:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Manabii wanatabiri uwongo,+

      Nao makuhani wanakandamiza kwa mamlaka yao wenyewe.

      Na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo.+

      Lakini mtafanya nini mwisho ukifika?”

  • Yeremia 6:12-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Watu wengine watapewa nyumba zao,

      Pamoja na mashamba yao na wake zao.+

      Kwa maana nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya wakaaji wa nchi,” asema Yehova.

      13 “Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+

      Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+

      14 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la watu wangu, wakisema,

      ‘Kuna amani! Kuna amani!’

      Wakati hakuna amani.+

      15 Je, wanaona aibu kwa sababu ya mambo yanayochukiza waliyotenda?

      Hawaoni aibu hata kidogo!

      Hata hawajui jinsi ya kufedheheka!+

      Basi wataanguka miongoni mwa wale walioanguka.

      Nitakapowaadhibu watajikwaa,” asema Yehova.

  • Yeremia 27:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “‘“‘Kwa hiyo, msiwasikilize manabii wenu, waaguzi* wenu, waota-ndoto wenu, wachawi wenu, na walozi wenu, wanaowaambia: “Hamtamtumikia mfalme wa Babiloni.”

  • Maombolezo 2:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Maono ambayo manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uwongo na yasiyofaa kitu,+

      Nao hawakufunua kosa lako ili kuzuia usipelekwe utekwani,+

      Bali waliendelea kukupa maono yenye ujumbe wa uwongo na unaopotosha.+

  • Ezekieli 22:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Lakini manabii wake wamepiga lipu matendo yao kwa kutumia chokaa. Wanaona maono ya uwongo na kufanya uaguzi* wa uwongo,+ nao wanasema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki