3 Kwa maana “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapowakusanya watu wangu waliotekwa, Israeli na Yuda,”+ asema Yehova, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao wataimiliki tena.”’”+
28 “‘Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao nitakapowapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa na kuwarudisha katika nchi yao, bila kumwacha yeyote kati yao huko.+