12 “Hata sasa,” asema Yehova, “rudini kwangu kwa mioyo yenu yote,+
Kwa kufunga+ na kulia na kuomboleza.
13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu,+
Nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu,
Kwa maana ni mwenye huruma na rehema, si mwepesi wa hasira,+ naye ana upendo mwingi mshikamanifu,+
Naye atafikiria upya msiba aliokusudia kuleta.
14 Ni nani ajuaye ikiwa hatabadili nia na kuufikiria upya+
Na kuwaachia baraka,
Ili mweze kumtolea Yehova Mungu wenu toleo la nafaka na toleo la kinywaji?