Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 30:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Sasa msiwe wakaidi kama mababu zenu.+ Jinyenyekezeni kwa Yehova, nanyi mje mahali pake patakatifu+ ambapo amepatakasa milele, mumtumikie Yehova Mungu wenu, ili hasira yake inayowaka iwaondokee.+ 9 Kwa maana mkirudi kwa Yehova, ndugu zenu na wana wenu wataonyeshwa rehema na wale waliowateka,+ nao wataruhusiwa kurudi katika nchi hii;+ kwa maana Yehova Mungu wenu ni mwenye huruma* na rehema,+ naye hataugeuza uso wake mbali nanyi mkirudi kwake.”+

  • Yeremia 18:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wakati wowote nitakaposema kuhusu kung’oa na kubomoa na kuharibu taifa au ufalme,+ 8 na taifa hilo liache uovu wake niliotangaza dhidi yake, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu msiba niliokusudia kuuleta dhidi yake.+

  • Sefania 2:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Kabla amri haijatekelezwa,

      Kabla siku hiyo haijapeperuka kama makapi,

      Kabla hasira inayowaka ya Yehova haijaja juu yenu,+

      Kabla siku ya hasira ya Yehova haijaja juu yenu,

       3 Mtafuteni Yehova,+ ninyi nyote mlio wapole* wa dunia,

      Mnaoshika amri zake za uadilifu.*

      Utafuteni uadilifu, utafuteni upole.*

      Huenda* mtafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki